WITO UMETOLEWA KWA WANANCHI HAPA NCHINI KUZINGATIA UPIMAJI WA ARDHI

TAREHE 01-10-2017

NAIBU WAZIRI WA ARDHI  NA MAENDELEO YA MAKAZI MH. ANGELINA MABULA

Serikali kupitia wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi  imetoa wito kwa wananchi wote hapa  nchini kuzingatia upimaji wa ardhi ili kusaidia kupatikana kwa makazi bora na yaliyopangwa.

Wito huo umetolewa  leo na naibu waziri wa Ardhi nyumba maendeleo na makazi Mh  Agelina Mabula wakati akizungumza  katika maadhimisho ya siku ya Makazi Duniani yaliyofanyika jijini Dar-es-salaam.

Amesema kuwa endapo wananchi watazingatia sheria ya makazi ya watu  pamoja na ya  ardhi kutawaepusha adha ya kusumbuliwa na kubomolewa  nyumba zao pale watakapobainika kuwa wamejenga maeneo yasiyoruhusiwa na serikali.


Ameongeza kuwa serikali kwa hivi sasa imejipanga  kuhakikisha kila mwananchi anakuwa kwenye makazi yaliyo bora na hii itaepusha  adha ya ujenzi usiofuata sheria  kwa baadhi ya mikoa hapa nchini kwa kuwa  wapo baadhi ya  wananchi ambao wamekosa elimu  namna ya kuwa na mipangilio mizuri ya iliyo makazi yao
WITO UMETOLEWA KWA WANANCHI HAPA NCHINI KUZINGATIA UPIMAJI WA ARDHI WITO  UMETOLEWA  KWA WANANCHI  HAPA NCHINI KUZINGATIA  UPIMAJI WA ARDHI Reviewed by safina radio on October 02, 2017 Rating: 5

No comments