HUDUMA YA KESHO JUMANNE KATIKA UKUMBI WA RADIO SAFINA
TAREHE 02-10-2017
Imeelezwa kukaa mbele
za Mungu kwa muda mrefu kunamfanya mtu aendelee kujiimarisha zaidi katika kila
eneo ikiwa ni pamoja na kuidhibiti milango ya adui.
Huduma ya Redio Safina
mkoani Arusha imekuandalia maombi maaliumu yakujifunza umuhimu wa kukaa mbele
za Mungu kwa muda mrefu maombi ambayo yatafanyika katika ukumbi uliopo Mbauda
kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita na nusu mchana.
Aidha, kwa kadiri unavyo
kaa mbele za Mungu kwa muda Mrefu ndivyo unavyo tengeneza mahusiano mazuri
baina yako wewe na Mungu.
Jumanne hii pia
tutamshughulikia yule adui azuiaye baraka zako katika maeneo mbalimbali kama
vile biashara ,elimu, kilimo, ufugaji, afya na hata ndoa sambamba na familia
kwa ujumla.
Hata hivyo, unaalikwa
wewe na jirani yako jumanne hii ili kukutana na muujiza wako ambapo watumishi
wamejipanga kikamilifu kuhakikisha kila atakaye hudhuria katika maombi hayo
anafunguliwa kila kifungo kinacho mkabili.
HUDUMA YA KESHO JUMANNE KATIKA UKUMBI WA RADIO SAFINA
Reviewed by safina radio
on
October 02, 2017
Rating:

No comments