MANISPAA YA DODOMA YAFANIKIWA KUJENGA DAMPO LA KISASA LA TAKA
TAREHE 17-10-2017
Manispaa ya Dodoma imefanikiwa kujenga dampo la kisasa la taka
ambalo lina uwezo wa kupokea tani 310 za taka huku likiwa na uwezo wa
kuzalisha ajira kwa wakazi wa manspaa hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika dampo hilo
la Chidaya mhandisi msimamizi wa dampo hilo bwana Barnabas Faida amesema kuwa
dampo hilo linaendeshwa kwa kutumia mitambo hali inayosaidia kuweka mji wa Dodoma katika hali ya usafi.
Amesema kuwa ujenzi wa dampo hilo la kisasa umetumia kiasi cha
zaidi ya bilioni mbili ambapo ujenzi wake ulianza mwaka 2011/2012 na kumalizika
2014 ambapo baada ya kumalizika lilianza rasmi kutumika mwaka 2016 ambapo
uendeshaji wake unatumia mitambo minne na hivyo kuwezesha kukabiliana na taka
zote zinazoingia katika dampo hilo.
Ameongeza kuwa kupitia dampo hilo limewezesha pia uzalishaji wa
ajira kwa wakazi wa Dodoma kwani kwa mwezi wanalazimika kutumia kiasi cha
shilingi milioni 20 kwa ajili ya kulipa vibarua na hivyo kuwezesha wakazi
hao kuweza kukabiliana na hali ngumu ya maisha..
Akizungumza kuhusiana na dampo hilo wasafirishaji wa taka
akiwemo Bw Godgery Chorobi amesema kuwa pamoja na kuwa dampo hilo lina
faida kwa kutoa ajira ingawa bado
wanakabliwa na changamoto ya ubovu wa barabara ya upelekaji taka katika dampo
hilo kutokana na miundombinu kuwa mibovu.
MANISPAA YA DODOMA YAFANIKIWA KUJENGA DAMPO LA KISASA LA TAKA
Reviewed by safina radio
on
October 17, 2017
Rating:

No comments