ARGENTINA HATARINI KUKOSA KOMBE LA DUNIA NCHINI URUSI

06-10-2017
Argentina, na mshambuliaji wao nyota Lionel Messi, wamo hatarini ya kukosa kufuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1970 baada ya kutoka sare tasa na Peru.
Ni nchi nne pekee za Amerika Kusini ambazo zinahakikishiwa nafasi katika michuano hiyo itakayofanyika Urusi mwaka 2018.
Argentina wamo katika nafasi ya sita wakiwa wamesalia na mechi moja pekee.
Mabingwa hao wa dunia mara mbili ni lazima washinde mechi yao ya mwisho ya kufuzu dhidi ya Ecuador kuwawezesha kufika angalau nafasi ya tano ambayo itawapatia fursa ya kucheza mechi mbili za muondoano za kufuzu dhidi ya New Zealand.
Mkufunzi wa Argentina Jorge Sampaoli amekiri kwamba mambo si mazuri lakini akaongeza kwamba ana imani kuwa iwapo timu hiyo itacheza ilivyocheza dhidi ya Peru, basi watafuzu kwa Kombe la Dunia.
Hata hivyo kocha Sampaoli amesifu bidii ya mchezaji  wa Barcelona ambaye aliunda nafasi nyingi sana za kufunga ingawa wenzake walishindwa kufunga.
Argentina, ambao walimaliza wa pili Kombe la Dunia 2014, wanalingana  kwa alama na Peru walio nafasi ya tano, alama 25.

Peru hata hivyo wako mbele kwa sababu wamefunga mabao mengi.

ARGENTINA HATARINI KUKOSA KOMBE LA DUNIA NCHINI URUSI ARGENTINA  HATARINI  KUKOSA KOMBE LA DUNIA NCHINI URUSI Reviewed by safina radio on October 06, 2017 Rating: 5

No comments