KABURI LENYE MIILI YA WATU WASIOPUNGUA 37 LAGUNDULIKA HUKO LIBYA

TAREHE 27-10-2017


Kaburi la umati lenye miili ya watu wasiopungua 37 limegunduliwa katika viunga vya mji wa Benghazi nchini Libya.

Maiti zilizogunduliwa katika kaburi hilo zimefungwa mikono kwa kamba na zina alama za kupigwa risasi.

Kaburi hilo limegunduliwa katika eneo lisilokuwa na makazi ya watu katika kitongoji cha Abyar kinachodhibitiwa na wapiganaji wa Jenerali mstaafu Khalifa Haftar.

Baadhi ya ripoti zinasema miili iliyokutwa katika kaburi hilo ni ya askari waliokuwa wakishikiliwa katika jela inayodhibitiwa na jeshi la Haftar tangu miezi kadhaa ilkiyopita.


Libya inasumbuliwa na machafuko makubwa ya kisiasa na kiusalama yaliyoanza baada ya kuondolewa madarakani kiongozi wa zamani wa nchi hiyo Muammar Gaddafi.
KABURI LENYE MIILI YA WATU WASIOPUNGUA 37 LAGUNDULIKA HUKO LIBYA KABURI  LENYE  MIILI  YA WATU  WASIOPUNGUA 37 LAGUNDULIKA  HUKO LIBYA Reviewed by safina radio on October 27, 2017 Rating: 5

No comments