USAJILI WA ELA NYINGI WAMFUKUZISHA KAZI KOEMAN

TAREHE 27-10-2017
Arsenal striker Olivier GiroudHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image c
Aliyekuwa meneja wa Everton Ronald Koeman amesema kuwa kushindwa kwake kumsaini mshambuliaji Olivier Giroud msimu huu kulichangia kufutwa kwake.
Koeman alifwa siku ya Jumamosi huku Everton wakiwa nafasi ya tatu kutoka mkia.
Anasema Giround, 31, alikaribia kukubali kuhamia Goodison Park.
Everton ilimuuza mfungaji wao bora zaidi Romelu Lukaku, kwenda Manchester United mwezi Julai katika makubaliano ya kima cha pauni milioni 75.
"Lukaku alikuwa muhumu kwetu, sio tu kwa magoli yake, lakini jinsi alikuwa akicheza," alisema Koeman.
Everton ilitumia pauni milioni 150 kumununua mchezaji wa kiunga cha kati Gylfi Sigurdsson kwa pauni milioni 45, Kipa Jordan Pickford kwa pauni milioni 30 na mlinzi Michael Keane kwa pauni milioni 30 na mchezaji wa kiungo cha kati Davy Klaassen kwa pauni milioni 24.
USAJILI WA ELA NYINGI WAMFUKUZISHA KAZI KOEMAN USAJILI  WA ELA NYINGI WAMFUKUZISHA  KAZI KOEMAN Reviewed by safina radio on October 27, 2017 Rating: 5

No comments