RAIS WA TANZANIA MH. MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAJUMBE WA SERIKALI ZA MITAA ALAT
TAREHE 03-10-2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amewataka wajumbe wa Jumuiya inayounganisha serikali za mitaa nchini ALAT kuungana kwa pamoja kudhibiti mianya inayopoteza mapato yanayotokana na raslimali za nchi ili kuwanufaisha wananchi wa hali ya chini pamoja na nchi kwa ujmla.
![]() |
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amewataka wajumbe wa Jumuiya inayounganisha serikali za mitaa nchini ALAT kuungana kwa pamoja kudhibiti mianya inayopoteza mapato yanayotokana na raslimali za nchi ili kuwanufaisha wananchi wa hali ya chini pamoja na nchi kwa ujmla.
Rais Magufuli ametoa wito huo leo
katika mkutano mkuu wa ALAT uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Julias Nyerere
jijini Dar es salaam ambapo amesema adui wa maendeleo ni kukosa umoja na
kuendekeza rushwa na ubadhirifu wa mali unaofanywa na baadhi ya watu wasio
waaminifu.
Aidha Dk Magufuli
ameeleza kuwa Tanzania imekuwa ikipoteza kiasi kikubwa cha kodi kutokana
ubebaji holela wa madini na usainishwaji wa mikataba inayofanywa na baadhi ya
watu na makampuni yanayojishughulisha na uchimbaji huo wa madini nakusema kuwa tangu
madini aina ya Tanzanite yaanze kuchimbwa Tanzania imepata asilimia tano ya
mapato ya madini hayo.
Licha ya
hayo Rais Magufuli ameeleza kuwa Serikali imepiga hatua kubwa katika miradi ya
maendeleo ya kijamii na kiuchumi hususani katika nyanja za elimu,miundombinu ya
barabara, afya, ikiwemo uagizaji wa madawa na vifaa tiba kutoka viwandani, maji
ambapo kumezinduliwa ya miradi ya maji katika halmashauri za miji na vijijini katika
mikoa mbalimbali hapa nchini.
RAIS WA TANZANIA MH. MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAJUMBE WA SERIKALI ZA MITAA ALAT
Reviewed by safina radio
on
October 03, 2017
Rating:

No comments