IGP SIMON SIRRO AWATAKA WANASASIASA KUACHA KUINGILIA MAJUKUMU YA JESHI LA POLISI

TAREHE 06-10-2017

Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka wanasiasa kuacha kuingilia majukumu ya Jeshi la polisi juu ya upelelezi wa watuhumiwa wa shambulio la mbunge wa Singida Mashariki Mh. Tundu Antipasi Lissu.

IGP Sirro ametoa kauli hiyo Mkoani Njombe kufuatia kuwepo kwa baadhi ya Wabunge kukosoa kauli yake aliyoitoa akiwa mkoani Mtwara ya kumtaka dereva wa Mbunge huyo kuripoti kwa ajili ya kutoa taarifa kuhusu upelelezi wa tukio la kujeruhiwa kwa Mbunge huyo.

Amesema  kuwa Jeshi hilo linaendelea na upelelezi ili kupata ushahidi unaojitosheleza na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano ili kurahisisha  upatikanaji wa taarifa hizo.


Aidha katika hatua nyingine, IGP Sirro amesema njia ya kumaliza mauaji yanayohusishwa na imani za kishirikina ni elimu kutolewa kwa wananchi kuupitia vyombo vya habari na nyumba za ibada kutokana na kuripotiwa kwa vitendo vya kiuhalifu vinavyohusishwa na imani za kishirikina, visasi na ubakaji  mkoani  Njombe.
IGP SIMON SIRRO AWATAKA WANASASIASA KUACHA KUINGILIA MAJUKUMU YA JESHI LA POLISI IGP  SIMON  SIRRO AWATAKA  WANASASIASA   KUACHA  KUINGILIA  MAJUKUMU YA JESHI LA POLISI Reviewed by safina radio on October 06, 2017 Rating: 5

No comments