BOTI ILIYOBEBA WAKIMBIZI YAZAMA USIKU WA KUAMKIA
TAREHE 09-10-2017
Boti
iliyokuwa imewabeba wakimbizi wa jamii ya Rohingya wanaokimbia machafuko katika
jimbo la Rakhine nchini Myanmar imezama usiku wa kuamkia leo karibu na pwani ya
Bangladesh na kusababisha watu wawili kufa maji na wengine kadhaa hawajulikani
walipo.
Walinzi
na maafisa wa pwani wamesema boti hiyo ilikuwa imefurika watu karibu 100 wakati
ilipozama katika mto Naf unaoitenganisha Myanmar na taifa jirani la Kusini mwa
Asia, Bangladesh.
Operesheni
ya uokozi imeendelea asubuhi hii na idadi ya watu ambao wamekosekana
haijatambulika.
Zaidi ya wakimbizi laki tano wa jamii ya wachache ya waislamu wa Rohingya
wameikimbia Myanmar tangu Agosti 25 wakati wanamgambo wa Rohingya
walipowashambulia polisi na jeshi katika jimbo la Rakhine na baadaye
kudhibitiwa katika operesheni kali na vikosi vya usalama vya Myanmar.
BOTI ILIYOBEBA WAKIMBIZI YAZAMA USIKU WA KUAMKIA
Reviewed by safina radio
on
October 09, 2017
Rating:

No comments