WATU WANNE WAMEUAWA KATIKA VURUGU ZA UCHAGUZI NCHINI KENYA

TAREHE 27-10-2017



Takriban watu wanne wameuwawa katika vurugu za uchaguzi nchini Kenya huku Kura zikiendelea kuhesabiwa katika kituo kikuu cha kujumlisha kura katika ukumbi wa Bomas jijini Nairobi baada ya  marudio ya uchaguzi wa urais yalifanyika hapo jana.

Hali ya kutokuwepo na usalama imesababisha kuahirishwa kwa uchaguzi katika kaunti nne huku maafisa wa uchaguzi wakisema kuwa zoezi hilo lilifanyika kwa amani na kama lilivyopangwa.

Tume ya uchaguzi nchini Kenya inakadiria kuwa asilimia 40 ya wapiga kura walijitokeza kushiriki katika zoezi hilo ikilinganishwa na asilimia 80 ya wapiga kura walioshiriki katika uchaguzi uliofanyika Agosti 8 na ambao ulibatilishwa na mahaka ya juu ya nchini humo.


Wafuasi wa upinzani hawakushiriki kwenye uchaguzi wa jana baada ya kiongozi mkuu wa upinzani Raila Odinga kuwatolea mwito wafuasi wa upinzani wasishiriki kwenye zoezi la kupiga kura.
WATU WANNE WAMEUAWA KATIKA VURUGU ZA UCHAGUZI NCHINI KENYA WATU  WANNE  WAMEUAWA KATIKA VURUGU  ZA UCHAGUZI  NCHINI  KENYA Reviewed by safina radio on October 27, 2017 Rating: 5

No comments