JIMBO LA KATALONIA NCHINI UHISPANIA LAENDELEZA HARAKATI ZA KUTAKA KUJITENGA

TAREHE 02-10-2017



Jimbo la Kaskazini Mashariki mwa Uhispania, Catalonia,lenye idadi ya watu milioni 7.5 na lenye utajirri mkubwa unaolingana na wa nchi ya Ureno limepiga kura ya maoni kujitenga na Serikali Kuu ya Uhispania

Kiongozi wa Jimbo hilo Bw.Carles Puigdemont amasema kuwa eneo la Uhispania limepata haki ya kuwa huru kufuatia kura ya maoni yenye utata ambayo imekumbwa na ghasia.

Maafisa wa Jimbo hilo la Catalonia wamesema kuwa asilimia 90 ya wale walioapiga kura wameunga mkono uhuru wa Jimbo lao katika kura ya maoni ya hapo jana jumapili.


Hata hivyo Mahakama ya katiba nchini Uhispania imeitangaza kura hiyo ya maoni kuwa kinyume na sheria,ambapo pia mamia ya watu wamejeruhiwa wakati polisi walitumia nguvu kujaribu kuzuia zoezi hilo.
JIMBO LA KATALONIA NCHINI UHISPANIA LAENDELEZA HARAKATI ZA KUTAKA KUJITENGA JIMBO    LA   KATALONIA   NCHINI  UHISPANIA    LAENDELEZA HARAKATI ZA KUTAKA KUJITENGA Reviewed by safina radio on October 02, 2017 Rating: 5

No comments