MKANDARASI ANAYEJENGA BARABARA YA GOBA MADALE DAR ES SALAAM ATAKIWA KUZINGATIA VIWANGO

TAREHE 04-10-2017

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO MH. MAKAME MBARAWA  MNYAA
Waziri wa ujenzi,uchukuzi na mawasiliano Mh Makame Mbarawa amewataka wakandarasi wanaojenga barabara ya Goba Madale jijini Dar-es-salaam kuzingatia viwango na ubora katika ujenzi wa barabara hiyo ili idumu kwa muda mrefu.

Mh Mbarawa ameyasema hayo baada ya kutembelea mradi maaulumu wa ujenzi barabara zilizoko pembezoni mwa jiji la Dar-es-salaam,ambapo amesema kuwa kampuni inayojenga barabara hiyo ni ya Kitanzania inayoitwa MICO na  inapaswa kujenga katika kiwango kinachokubalika na si kufanya ubabaishaji.

Amesema kuwa,serikali pamoja na wananchi wanataka waone barabara hiyo inakamilika kwa viwango na kama itakamilika kama walivyokubaliana kampuni hiyo itaendelea kupewa kazi nyingi zaidi na serikali lengo likiwa ni kuziwezesha kampuni za ndani.


Kwa upande wake mratibu wa mradi kutoka kampuni hiyo ya Mico Bw Crispin Mwombeki amesema kuwa changamoto kubwa inayokabili kampuni hiyo ulipaji wa fidia walioko kandokando ya barabara.
MKANDARASI ANAYEJENGA BARABARA YA GOBA MADALE DAR ES SALAAM ATAKIWA KUZINGATIA VIWANGO MKANDARASI  ANAYEJENGA  BARABARA    YA   GOBA   MADALE   DAR ES SALAAM    ATAKIWA   KUZINGATIA   VIWANGO Reviewed by safina radio on October 04, 2017 Rating: 5

No comments