IGP SIMON SIRRO AMESEMA BIASHARA NA UTUMIAJI WA MADAWA YA KULEVYA IMEPUNGUA HAPA NCHINI
TAREHE 09-10-2017
Mkuu wa jeshi la polisi hapa nchini IGP Saimon Sirro
amesema kuwa biashara na utumiaji wa madawa ya kulevya imepungua kwa kiasi
kikubwa hapa nchini kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na vyombo vya dola
kudhibiti biashara hiyo.
IGP Sirro ameyasema hayo wakati akizungumza na
kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mbeya katika ziara yake ya kutembelea
mikoa ya nyanda za juu kusini yenye lengo la kuangalia hali ya usalama katika
mikoa hiyo.
Amesema kuwa tangu kuanza kwa operesheni ya kupambana
na biashara ya dawa za kulevya hapa nchini watumiaji wake wamepungua kwa kiasia
kikubwa,na jeshi la polisi litaendelea kuwakamata wale wote wanaojihusisha na
dawa hizo bila kujali uwezo wake wa kifedha wala cheo chake.
Aidha katika hatua nyingine mkuu huyo wa polisi
ameviagiza vikosi vya jeshi hilo vilivyoko maeneo ya mipakani kuwachukulia
hatua kali za kisheria wafanyabiashara wanaokwepa kulipa kodi.
Amesema kuwa wafanyabishara wanapokwepa kulipa kodi
wanasababisha serikali kupata mapato yake hivyo kuanzia sasa jeshi la polisi
limejipanga kuwafikisha katika vyombo vya dola wafanyabiashara wote wanaokwepa
kodi.
IGP SIMON SIRRO AMESEMA BIASHARA NA UTUMIAJI WA MADAWA YA KULEVYA IMEPUNGUA HAPA NCHINI
Reviewed by safina radio
on
October 09, 2017
Rating:

No comments