SEKTA BINAFSI HAPA NCHINI ZATAKIWA KUWASILIANA MOJA KWA MOJA NA SERIKALI
TAREHE 25-10-2017
![]() |
WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO DK. PHILIP MPANGO |
Sekta
binafsi hapa nchini imetakiwa kuwasiliana moja kwa moja na serikali ili kutatua
changamoto zinazowakabili badala ya kupitia wakala wa nje kwanza kwa kuwa
mlango wa serikali uko wazi kwa ajili ya majadiliano na kutatua matatizo ya
sekta hiyo.
Rai hiyo
imetolewa na jijini Dar es salaam na Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip
Mpango katika Mkutano na sekta binafsi nchini TPSF,ambapo amesema kuwa ni vema
sekta binafsi ikashirikiana na sekta ya umma kwa kuwa zote zinategemeana na hakuna
nchi iliyoendelea bila kuwa na sekta binafsi ambayo ni imara.
Hata
hivyo, amesema lengo la pande zote mbili kukutana ni kuharakisha utekelezaji wa
azma ya serikali ya awamu ya tano kuongeza fursa za ajira, kipato cha wananchi,
kuondokana na umasikini uliokithiri kwa kuwa Tanzania inaongozwa na uchumi wa
viwanda.
SEKTA BINAFSI HAPA NCHINI ZATAKIWA KUWASILIANA MOJA KWA MOJA NA SERIKALI
Reviewed by safina radio
on
October 25, 2017
Rating:

No comments