ODINGA AMETOA WITO KWA WAFUASI WAKE KUENDELEA NA MAANDAMANO

TAREHE 16-10-2017

Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga, ambaye alijitoa  kwenye uchaguzi mpya wa urais wa hapo Oktoba 26, mwaka huu amewatolea wito wafuasi wake kuendelea na maandamano licha ya serikali kupiga marufuku maandamano hayo.


Serikali ya Rais Uhuru Kenyatta imepiga marufuku maandamano kwenye vitovu vya miji mikubwa, ikisema inazuia machafuko na uharibifu wa mali.
Akizungumza na maelfu ya wafuasi wake katika mji wa pwani wa Mombasa, Odinga ambaye juzi alikuwa London, Uingereza, amesema alikwenda huko kuzungumzia hasa kile kinachotokea sasa nchini Kenya.

Odinga na muungano wa upinzani wa NASA wanashinikiza kufanyika kwa marekebisho makubwa kwenye tume ya uchaguzi, IEBC, kabla ya kuitishwa uchaguzi mwengine.


Hata hivyo hadi sasa, watu wawili wanaripotiwa kupoteza maisha kwenye maandamano dhidi ya IEBC.
ODINGA AMETOA WITO KWA WAFUASI WAKE KUENDELEA NA MAANDAMANO ODINGA   AMETOA  WITO  KWA  WAFUASI   WAKE   KUENDELEA  NA  MAANDAMANO Reviewed by safina radio on October 16, 2017 Rating: 5

No comments