MAREKANI YAPELEKA MSAADA SOMALIA

TAREHE 18-10-2017


Ndege ya kijeshi ya Marekani imetua hii leo katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu ikiwa na misaada ya kiutu kufuatia shambulizi lililowaua zaidi ya watu 300 nchini humo.

Shambulizi hilo baya zaidi katika historia ya Somalia na moja ya mashambulizi mabaya ulimwenguni limewajeruhi kiasi cha watu mia nne ambapo Maafisa nchini humo wanasema watu kadhaa bado hawajulikani walipo na idadi ya vifo inaweza kuongezeka.

Wakati mazishi ya waliouawa yakiendelea watu kadhaa waliojeruhiwa vibaya wamepelekwa Uturuki kwa uangalizi zaidi kimatibabu, ambapo serikali ya Kenya imeahidi kuwasafirisha majeruhi 31 kutoka Somalia hadi Nairobi kwa ajili ya matibabau zaidi.


Hali kadhalika, Kenya imepeleka tani 11 za madawa na mahitaji mengine nchini Somalia,na Serikali ya Somalia inalishutumu kundi la al- Shabab kwa kuhusika na shambulizi hilo ingawa kundi hilo hadi sasa halijatoa tamko lolote.
MAREKANI YAPELEKA MSAADA SOMALIA MAREKANI   YAPELEKA   MSAADA   SOMALIA Reviewed by safina radio on October 18, 2017 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.