WAZIRI LUKUVI AMEWAAGIZA MAAFISA MIPANGO MIJI HAPA NCHINI KUTENGA MAENEO MAPYA YA UWEKEZAJI NA MAKAZI.
TAREHE 27-10-2017
Waziri wa
Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi amewaagiza Maafisa wa
Mipango Miji hapa nchini kutenga maeneo mapya ya makazi na maeneo ya uwekezaji
katika Halmashauri zao ili kufanikisha azma ya serkali kuelekea uchumi wa Viwanda.
Waziri
Lukuvi ameyasema hayo jijini Dar es salaam kwenye Mkutano wa Bodi ya Usajili wa
Wataalamu wa Mipango Miji na kuwataka wataalamu hao kutatua changamoto katika
ufuatiliaji wa maendeleo ya mipango miji.
Aidha, Waziri
Lukuvi ameongeza kwa Mkutano huo uwe kama Jukwaa la kubadilishana uzoefu,
maarifa na mbinu mpya za kuandaa mipango miji itakayofanikisha uwekezaji wa
maendeleo endelevu za viwanda kwa kuwa serikali ya awamu ya tano imeamua kuweka
msisitizo kwenye uwekezaji wa viwanda.
Kwa
upande Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prf. Wilbert Kombe amesema changamoto
inayowakabili ni ukosefu wa rasilimali watu katika maeneo mengi ya miji.
Hata
hivyo Mkutano wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Mipango Miji umewahusisha
Wajumbe wa bodi hiyo pamoja na Wataalamu Mipango wa Miji kutoka Halmashauri
mbalimbali hapa nchini.
WAZIRI LUKUVI AMEWAAGIZA MAAFISA MIPANGO MIJI HAPA NCHINI KUTENGA MAENEO MAPYA YA UWEKEZAJI NA MAKAZI.
Reviewed by safina radio
on
October 27, 2017
Rating:

No comments