MKUU WA MKOA WA TANGA BW. MARTIN SHIGELLA AIOMBA TANESCO MKOANI HUMO KUONGEZA MIUNDOMBINU.

TAREHE 06-10-2017


Mkuu wa mkoa wa Tanga Bw Martin Shigela ameliomba shirika la umeme Tanzania TANESCO kuongeza miundombinu ya kutosha kwa ajili kusambaza umeme wa kutosha ili kukidhi mahitaji  kwa  siku za hivi karibuni  kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo Mkoani humo.

Shigela ametoa ombi hilo wakati akifungua  mkutano wa 47 wa Baraza Kuu la wafanyakazi  wa TANESCO uliofanyika huko Tanga ambapo amesema Serikali inaendelea na mchakato wa kuimarisha miundombinu ya usafirishaji wa umeme 

Aidha, Shingela ameongeza kuwa miongoni mwa miradi mikubwa  ya uwekezaji unaohitaji  umeme wa kutosha ni ujenzi wa bomba la mafuta unaoendelea kutokana na kazi kubwa ya uunganishaji  na uvalishwaji wa mabomba hayo.

Vile vile, Shingela ameongeza kuwa umeme unahitajika kutokana na uwepo wa ujenzi  wa viwanda ambapo kiwanda kimoja kinakadiriwa kuzalisha takribani tani milioni saba kwa mwaka na kuwapo kwa mahitaji ya uzalishaji wa simenti na nondo kwa wingi kutoka kwenye viwanda vingine kwa ajili ya ujenzi  wa viwanda hivyo huku kukiwa na uzalishaji wa nguzo za zege zinazohitaji nondo na simenti.


Hata hivyo, Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO utafanyika kwa siku mbili.
MKUU WA MKOA WA TANGA BW. MARTIN SHIGELLA AIOMBA TANESCO MKOANI HUMO KUONGEZA MIUNDOMBINU. MKUU WA MKOA WA TANGA  BW. MARTIN  SHIGELLA  AIOMBA  TANESCO MKOANI HUMO KUONGEZA  MIUNDOMBINU. Reviewed by safina radio on October 06, 2017 Rating: 5

No comments