RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP AMEMWAMBIA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA TAIFA HILO KUWA ANAPOTEZA MUDA WAKE KUFANYA MAZUNGUMZO NA KOREA YA KASKAZINI
TAREHE 02-10-2017
![]() |
RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP |
Rais wa Marekani Donald Trump
amemuambia waziri wake wa mashauri ya nchi za nje Bw. Rex Tillerson kuwa
anapoteza muda wake akijaribu kufanya mazungumzo na Korea Kaskazini kuhusu
mpango wake wa nyuklia.
Bw.Tillerson alifichua hayo siku ya
Jumamosi akisema kuwa Korea Kaskazini haitilii maanani mazungumzo hayo.
Marekani inataka Korea Kaskazini
kusitisha mipango yake ya silaha baada ya kufanya majaribio kadha ya makombora
ya Nyuklia na kudai kufanya jaribo la bomu la haidrojeni ambalo linaweza
kutundikwa kwa kombora la masafa marefu.
Mh. Trump, alisema kuwa jeshi la
Marekani lilikuwa tayari kukabiliana na Korea Kaskazini mapema Mwezi Agost, saa
chache baada ya waziri wake wa ulinzi kujaribu kutuliza misukosuko akisema kuwa
jitihada za mazungumzo zilikuwa zinafanikiwa.
Matamshi ya rais Trump yanakuja siku
moja baada ya Bw. Tillerson kufichua kuwa maafisa wa Marekani walikuwa na
mawasiliano na Korea Kaskazini licha ya kuwepo vita vya maneno kati ya viongozi
wa nchi hizo mbili.
RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP AMEMWAMBIA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA TAIFA HILO KUWA ANAPOTEZA MUDA WAKE KUFANYA MAZUNGUMZO NA KOREA YA KASKAZINI
Reviewed by safina radio
on
October 02, 2017
Rating:

No comments