UFARANSA KUWAPA HIFADHI WAKIMBIZI ELFU KUMI

TAREHE 10-10-2017

Serikali ya Ufaransa inapanga kuwaruhusu jumla ya wakimbizi elfu kumi kutoka nchi kadhaa zisizo  za  Ulaya kuingia nchini humo kihalali katika kipindi cha miaka miwili ijayo kama sehemu ya mpango ya kuwapa makazi wakimbizi.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema watashirikiana na ofisi ya kamishna mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu  kuwaruhusu wakimbizi kutoka Uturuki, Jordan, Niger na Chad kuingia Ufaransa.

Halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya iliwasilisha mpango mpya wa kuwapa wakimbizi hifadhi wiki mbili zilizopita ambao utaruhusuu wakimbizi elfu hamsini kupata hifadhi Ulaya katika kipindi cha miaka miwili ijayo.


 Umoja wa Ulaya umesema mpango huo mpya utawalenga watu walio katika mazingira hatari kutoka Libya, Misri, Niger, Sudan, Chad na Ethiopia mbali na wanaotoka Uturuki na kanda ya Mashariki ya Kati.
UFARANSA KUWAPA HIFADHI WAKIMBIZI ELFU KUMI UFARANSA KUWAPA HIFADHI WAKIMBIZI ELFU KUMI Reviewed by safina radio on October 10, 2017 Rating: 5

No comments