ZAIDI YA WATU 50 WAMEUAWA NCHINI MAREKANI


TAREHE 02-10-2017
Zaidi ya watu 50 wameuawa na takriban 200 kujeruhiwa kwenye ufyatuaji wa risasi wakati wa tamasha la muziki huko Las Vegas, nchini Marekani.
Mtu mwenye bunduki mwenye umri wa maiaka  64 Stephen Paddock alifyatua risasi kutoka ghoroga ya 32 kwenye hoteli ya Mandalay Bay, wakati tamasha  likiendelea nje.
Polisi wanasema mshukiwa ambaye alitajwa kuwa mkaazi wa mji huo na ambaye hakutajwa jina ameuawa.
Mamia ya watu walikimbia eneo hilo na milio ya risasi ikasikika kwa muda kwenye video zilizochapishwa katika mitandao ya kijamii.
Ufyatuaji huo ulitokea mwendo wa saa 05:30 usiku  na walioshuhudia walisema kuwa mamia ya risasi zilifyatuliwa.

Usafiri wa ndege ulisitishwa kutoka uwanja wa ndege wa Mc Carran mjini Las Vegas.
ZAIDI YA WATU 50 WAMEUAWA NCHINI MAREKANI ZAIDI YA WATU 50 WAMEUAWA NCHINI MAREKANI Reviewed by safina radio on October 02, 2017 Rating: 5

No comments