SERIKALI KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOKABILI ASASI BINAFSI ZINAZOHUSIKA NA UHIFADHI WA WANYAMAPORI

TAREHE 25-10-2017


Serikali imeahidi kutatua changamoto zinazozikumba asasi binafsi zinazohusika na uhifadhi wa wanyama pori ili kuleta maendeleo baina ya pande zote mbili .

Hayo yamesemwa na Katibu mkuu wa wizara ya mali asili na utalii  Meja jenerali Gaudence Milanzi jijini Dar es salaam baada ya kushiriki kikao na asasi binafsi ishirini na tano zinazohusika na uhifadhi wa wanyama pori nchini.

Kwa upande wake mkurugenzi  idara ya wanyama pori wizara ya mali asili na utalii, Profesa Alexanda Songorwa amesema kuwa wizara hiyo ina matarajio ya kusonga mbele katika kuhifadhi wanyama pori.


Hata hivyo katika kikao hicho wadau wa uhifadhi wa wanyama pori wamehimizwa kushiriki vyema katika shughuli za kijamii kwenye maeneo waliyowekeza ikiwemo kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili jamii inayowazunguka..
SERIKALI KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOKABILI ASASI BINAFSI ZINAZOHUSIKA NA UHIFADHI WA WANYAMAPORI SERIKALI KUTATUA  CHANGAMOTO ZINAZOKABILI ASASI BINAFSI ZINAZOHUSIKA NA UHIFADHI WA  WANYAMAPORI Reviewed by safina radio on October 25, 2017 Rating: 5

No comments