MKANDARASI ANAYEJENGA BARABARA KUTOKA SUMBAWANGA HADI KASANGA ATAKIWA KUKAMILISHA KWA WAKATI
TAREHE 17-10-2017
Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amemwangiza Meneja wa Wakala wa Barabara TANROADS mkoa wa Rukwa
kuhakikisha kuwa Mkandarasi anayejenga barabara kwa kiwango cha lami kutoka
Sumbawanga hadi bandari ndogo ya Kasanga wilayani Kalambwe inakamilika kwa
wakati.
Prf. Mbarawa ametoa
agiza hilo Mkoani Rukwa wakati akikagua ujenzi wa barabara za lami Mkoani humo
na kusisitiza kuwa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita mia moja na kumi inatakiwa
kukamilika kabla ya mwezi septemba, 2018.
Kwa upande wake Meneja
wa TANROADS mkoani Rukwa Msuka Mkina amesema mkandarasi wa barabara hiyo China
Rellway Cooperation ameahidi kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.
Hata hivyo kukamilika
kwa barabara hiyo kunatajwa kuwa kichocheo kikubwa cha kufungua milango ya
kibiashara baina ya Tanzania na nchi za jirani.
MKANDARASI ANAYEJENGA BARABARA KUTOKA SUMBAWANGA HADI KASANGA ATAKIWA KUKAMILISHA KWA WAKATI
Reviewed by safina radio
on
October 17, 2017
Rating:

No comments