MGOMO WATISHIA KUKWAMISHA KAZI KATIKA JIMBO LA KATALONIA

TAREHE 03-10-2017

Mgomo mkubwa unatishia kukwamisha shughuli katika sehemu kubwa za Catalonia nchini Uhispania kufuatia kura ya maoni yenye utata.

Mgomo huo ulioitishwa na vyama vya wafanyakazi huko Catalonia, unalalamikia ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu ulioshuhudiwa wakati wa kura ya maoni siku ya Jumapili.

Uhispania imeitaja kura hiyo ya maoni kuwa iliyo kinyume na sheria huku raia waliopiga kura hiyo wakitajwa kuwa ni zaidi ya milioni 2.2 ambapo mimia yao walijeruhiwa wakati polisi wa Uhispania wakijaribu kuzuia zoezi hilo kutoendelea.

Baadhi ya maafisa walioamrishwa kuwazuia watu wasipige kura walionekana wakifyatua risasi za mipira, wakivamia vituo vya kupigia kura na kuwavuta wanawake nywele zao huk maafisa wa afya huko Catalonia wakisema kuwa Polisi 3 walijerihiwa siku ya Jumapili.


Habari zinaeleza kuwa mgomo huo wa leo Jumanne utavuruga shushuli za usafiri wa umma, shule na zahahati huko Catalonia ambapo Klabu maarufu cha mpira wa miguu cha Barcelona pia kikitarajiwa kugoma, licha ya kuwa hawachezi mechi huku vyuo vya umma na makavazi nayo yakitarajiwa kugoma.
MGOMO WATISHIA KUKWAMISHA KAZI KATIKA JIMBO LA KATALONIA MGOMO   WATISHIA   KUKWAMISHA KAZI KATIKA JIMBO LA KATALONIA Reviewed by safina radio on October 03, 2017 Rating: 5

No comments