VIONGOZI WAWILI WAFUNGWA NCHINI UHISPANIA KWA UCHOCHEZI

TAREHE 17-10-2017

Jaji wa mahakama moja nchini Uhispania ameamuru kufungwa kwa viongozi wawili wa vuguvugu linalounga mkono uhuru wa jimbo la Catalonia kwa mashitaka ya uchochezi.

Viongozi hao wanatuhumiwa kuwataka wafuasi wao kuwazuia polisi wasifanye uvamizi wakati wa kura ya maoni mwanzoni mwa mwezi huu, ambayo viongozi wa Catalonia wanasema takribani asimilia 90 ya wapiga kura waliunga mkono jimbo hilo kujitangazia uhuru kutoka Uhispania.

Jaji huyo amewatia hatiani viongozi hao kwa kutumia mitandao ya kijamii kuitisha maandamano.


Waziri Mkuu wa Uhispania, Mariano Rajoy, alimpa Rais Carles Puigdemont hadi kesho kutwa Alhamisi awe ameshaweka bayana endapo ametangaza uhuru wa jimbo hilo tajiri la kaskazini. 
VIONGOZI WAWILI WAFUNGWA NCHINI UHISPANIA KWA UCHOCHEZI VIONGOZI WAWILI WAFUNGWA NCHINI UHISPANIA KWA UCHOCHEZI Reviewed by safina radio on October 17, 2017 Rating: 5

No comments