KWA MUJIBU TAFITI ZILIZOFANYWA ZIMEONYESHA KUWA TAKRIBANI MIAKA 15 IJAYO KUTAKUWA NA UKOSEFU WA NYAMA NYEKUNDU
TAREHE 26-10-2017
Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi
Mh Abdallah Ulega amesema kuwa tafiti zilizofanywa na wataalam wa mifugo
zinaonyesha kuwa takribani miaka 15 ijayo kutakuwa na ukosefu wa nyama
nyekundu kutokana na kutofanyika kwa mikakati mahususi ya uwekezaji katika
mifugo na uvuvi.
Mh Ulega ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa siku tatu wa
wataalamu wa mifugo unaoendelea jijini Arusha ambao umelenga kubadilishana
mawazo na uzoefu kwa wataalamu hasa kwenye shughuli mbalimbali wanazozifanya
katika sekta ya mifugo na uvuvi.
Amesema kuwa nchini Tanzania
watu hufuga mifugo yao na kuizalisha kwa njia za kienyeji ambazo
haziwaletei manufaa hivyo amewataka wafugaji kufuga mifugo michache ambayo
itaweza kuwaletea faida wao binafsi na taifa kwa ujumla.
Aidha ameongeza kuwa mifugo na uzalishaji nyama iwe sehemu ya
mapambano ya kuwa na Tanzania ya viwanda kwa kuwa na nyama za uhakika katika
viwanda ili kuweza kutosheleza soko la ndani na kupunguza gharama za manunuzi
ambazo baadhi ya wananchi hushindwa kununua nyama kutokana na ukubwa wa
gharama.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha wataalamu wa mifugo
Tanzania Dkt. Daniel Komuyangiro amesema kuwa kupitia mkakati wa Tanzania of
máster plan serikali itaweza kuwekeza katika uzalishaji wa nyama nyeupe ambao
utawasaidia wafugaji kuondokana na umaskini sambamba na kupunguza mahitaji ya
nyama nchini.
KWA MUJIBU TAFITI ZILIZOFANYWA ZIMEONYESHA KUWA TAKRIBANI MIAKA 15 IJAYO KUTAKUWA NA UKOSEFU WA NYAMA NYEKUNDU
Reviewed by safina radio
on
October 26, 2017
Rating:

No comments