JESHI LA POLISI MKOANI ARUSHA LAPOKEA MSAADA WA SARUJI

TAREHE 10-10-2017

KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA  CHARLES MKUMBO

Jeshi la polisi Mkoani Arusha limepokea jumla ya mifuko elfu moja na mia tatu ya saruji kutoka kwa wadau mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa makazi mapya ya nyumba za polisi zilizoteketea kwa moto hivi karibuni. 

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea msaada huo kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Arusha Charles Mkumbo amewashukuru wadau hao kwa kujitoa kusaidia ujenzi huo.

Kamanda Mkumbo amesema msaada huo utawawezesha kwa kiwango kikubwa katika kukamilisha ujenzi wa nyumba za makazi ya familia 13 ambao pia walipoteza mali zao. 

Aidha ameyaomba makampuni mengine kuiga mfano huo wa kujitoa kwa moyo katika kusaidia ujenzi huo pamoja na jamii nyingine zenye uhitaji ili kuweza kuleta maendeleo katika Taifa.

Hata hivyo moto ulioteketeza nyumba hizo za askari  katika eneo la Sekei jijini Arusha ulitokea   mnamo Septemba 27 mwaka huu,ambapo siku moja baada ya janga hilo rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli alitoa kiasi cha shilingi milioni mia mbili sitini kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa majengo hayo.
JESHI LA POLISI MKOANI ARUSHA LAPOKEA MSAADA WA SARUJI JESHI  LA  POLISI  MKOANI  ARUSHA  LAPOKEA  MSAADA  WA  SARUJI Reviewed by safina radio on October 10, 2017 Rating: 5

No comments