VIONGOZI WA AFRIKA MAGHARIBI WAMETOA MAONI YAO JUU YA VURUGU ZINAZOENDELEA NCHINI TOGO

TAREHE26-10-2017

Viongozi wa Afrika Magharibi wametoa maoni yao ya kwanza baada ya miezi miwili ya vurugu mbaya zinazoendelea nchini Togo.

Viongozi hao wamemtaka rais wa Togo Faure Gnassingbe na upande wa upinzani kufanya mazungumzo ili kusuluhisha mgogoro wa kisiasa uliopo nchini humo.

Ufaransa pia imetoa mwito wa kufanyika majadiliano ya haraka baina ya pande hizo mbili katika nchi iliyokuwa zamani ni koloni lake na kusema kuwa ina wasiwasi kutokana na ripoti kwamba wapiganaji wa kiraia wanafanya kazi pamoja na vikosi vya usalama.

Takriban watu16 wameuawa na wengine wengi wamejeruhiwa katika maandamano ya kuipinga serikali.

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara amesema yeye na wenzake kutoka Nigeria, Niger na Ghana walikutana siku ya Jumanne na Rais wa Togo Faure Gnassingbe kujadili juu ya suala hilo.
VIONGOZI WA AFRIKA MAGHARIBI WAMETOA MAONI YAO JUU YA VURUGU ZINAZOENDELEA NCHINI TOGO VIONGOZI WA  AFRIKA  MAGHARIBI WAMETOA MAONI YAO JUU YA VURUGU ZINAZOENDELEA NCHINI TOGO Reviewed by safina radio on October 26, 2017 Rating: 5

No comments