JUHUDI ZA KIDIPLOMASIA KUENDELEA ILI KUTATUA MGOGORO WA KOREA KASKAZINI NA MAREKANI

TAREHE  16-10-201
WAZIRI  WA  MAMBO  YA NJE  WA  MAREKANI  REX  TILLERSON.

Waziri wa Mambo wa Nje wa Marekani, Rex Tillerson, amesema kuwa juhudi za kidiplomasia kuutatua mzozo wa Korea Kaskazini zitaendelea kabla nchi hiyo  haijachukua hatua za kijeshi.

Kauli  ya Bw  Tillerson inakuja hata baada ya Rais Donald Trump kutuma ujumbe kwenye mtandao wa Twitter wiki chache zilizopita, kwamba waziri wake huyo anapoteza muda kujadiliana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jung-Un, aliyemwita mtu wa maroketi.

Akizungumza kwenye kipindi cha State of the Union cha televisheni ya CNN hivi leo, Tillerson amesema huenda Trump anataka kuweka wazi kwa Kim Jung-Un kwamba upo mpango wa kijeshi kama diplomasia ikishindwa, lakini sio kwamba Marekani imeachana na juhudi hizo.


Hata hivyo mgongano huo wa kauli kutoka ngazi za juu katika serikali ya Trump umezua wasiwasi juu ya uwezekano wa kutopigwa hesabu vyema kwenye mzozo kati ya Marekani na Korea Kaskazini.
JUHUDI ZA KIDIPLOMASIA KUENDELEA ILI KUTATUA MGOGORO WA KOREA KASKAZINI NA MAREKANI JUHUDI  ZA   KIDIPLOMASIA  KUENDELEA  ILI KUTATUA  MGOGORO   WA  KOREA  KASKAZINI NA  MAREKANI Reviewed by safina radio on October 16, 2017 Rating: 5

No comments