WAZAZI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KWA KARIBU NA WAALIMU.

TAREHE 04-10-2017


Wazazi nchini wametakiwa kushirikiana kwa karibu na waalimu katika kuwahimiza na kuwalekeza watoto wao kusoma kwa bidii.

Wito huo umetolewa  na Afisa elimu wa Shule za Msingi Halmashauri ya Mji wa Babati, Bi. Doroth Mwandila wakati akizungumza  na wazazi na wanafunzi wa halmashauri hiyo  juu ya umuhimu wa kuwa karibu na  watoto wa shule ili kuongeza ufaulu na maadili katika jamii.

Mwandila amesema ili  kufikia azma ya maendeleo ya viwanda nchini yanayohamasishwa na Serikali ya awamu ya tano ipo haja ya wazazi kushirikiana na walimu ili kuzalisha kizazi kitakacho kuwa na elimu na wajibu wa kujituma.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Msingi Deira iliyopo wilayani Babati mkoani Manyara Daniel Gaitu amesema wameitikia wito wa kuwafundisha wanafunzi masomo ya sayansi ili kuzalisha wataalam watakaotumika katika miradi mbalimbali.  


Naye Mwanafunzi Edson Eliudi wa Shule ya Msingi Deira aliyeongoza nafasi ya kwanza kwenye mitihani ya majaribio iliyohusisha Shule 37 zilizopo Halmashauri ya Mji wa Babati amesema kuwa siri ya mafanikio yake ilitokana na wazazi wake kumfuatilia kimasomo na kuwa karibu naye pamoja na walimu.


WAZAZI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KWA KARIBU NA WAALIMU. WAZAZI   WATAKIWA  KUSHIRIKIANA   KWA  KARIBU  NA  WAALIMU. Reviewed by safina radio on October 04, 2017 Rating: 5

No comments