WAZIRI ANGELA KAIRUKI AITAKA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA KUIPATIA SERIKALI WATU WENYE SIFA
TAREHE 06-10-2017
Waziri wa nchi ofisi ya rais utumishi na utawala bora Mh Angela Kairuki ameitaka bodi ya sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma kuipatia serikali rasilimali watu wenye sifa stahiki weledi na uwezo wa kuwezesha serikali kutimiza malengo yake.
![]() |
WAZIRI ANGELA KAIRUKI |
Waziri wa nchi ofisi ya rais utumishi na utawala bora Mh Angela Kairuki ameitaka bodi ya sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma kuipatia serikali rasilimali watu wenye sifa stahiki weledi na uwezo wa kuwezesha serikali kutimiza malengo yake.
Mh Kairuki ametoa rai
hiyo wakati akizungumza katika uzinduzi wa bodi ya tatu ya sekretarieti ya
ajira katika utumishi wa umma jijini Dar-es-salaam,ambapo amesema kuwa dhamira
ya serikali ni kujenga utamaduni wa kutaka watu kuacha kufanya kazi kwa mazoea.
Amesema kuwa kila mmoja
anafahamu azma ya serikali ya kutaka kuingia katika uchumi wa kati na uchumi wa
viwanda kwa hiyo bodi hiyo ina majukumu makubwa sana kuliwezesha taifa kupata
rasilimali watu ambao wana weledi,uadilifu na uzalendo wa kutosha katika
kulitumikia taifa.
Kwa upande wake
mwenyekiti wa bodi hiyo Bi Rose Lugembe amesema kuwa watahakikisha wanazingatia
sheria kanuni na taratibu ili kuwezesha serikali kupata watumishi
watakaowezesha kupeleka gurudumu la
maendeleo mbele.
WAZIRI ANGELA KAIRUKI AITAKA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA KUIPATIA SERIKALI WATU WENYE SIFA
Reviewed by safina radio
on
October 06, 2017
Rating:

No comments