MGOMBEA URAIS NCHINI LIBERIA NA MWANASOKA WA ZAMANI WA TAIFA HILO GEORGE WEAH AKIRI KUWA NA MAWASILIANO NA RAIS WA ZAMANI CHARLES TAYLOR

TAREHE 06010-2017
GEORGE WEAH
Mmoja wa wagombea katika uchaguzi wa urais nchini Liberia na nyota wa soka George Weah amekiri kuwa na mawasiliano na kiongozi wa zamani wa taifa hilo Charles Taylor.
Bw Taylor anatumikia kifungo cha miaka 50 jela nchini Uingereza kwa makossa uhalifu wa kivita baada ya kuhukumiwa na mahakama maalum ya Umoja wa Mataifa.
Bw Weah amesema kuwa alipokea simu kutoka kwa mbabe huyo wa kivita, lakini akakanusha kwamba Charles Taylor ana ushawishi wa mambo nchini humo.
Wiki iliyopita, Bunge la Congress nchini Marekani liliidhinisha azimio la kushutumu juhudi zozote za mbabe huyo wa zamani wa kivita za kujaribu kuwa na ushawishi kwenye uchaguzi nchini Liberia kutoka gerezani.

Hata hivyo George Weah ni mmoja wa wagombea 11 ambao wamejitokeza kutaka kumrithi Rais Ellen Johnson-Sirleaf ambaye anastaafu.
MGOMBEA URAIS NCHINI LIBERIA NA MWANASOKA WA ZAMANI WA TAIFA HILO GEORGE WEAH AKIRI KUWA NA MAWASILIANO NA RAIS WA ZAMANI CHARLES TAYLOR MGOMBEA   URAIS NCHINI  LIBERIA  NA MWANASOKA  WA ZAMANI  WA TAIFA  HILO  GEORGE WEAH  AKIRI  KUWA NA MAWASILIANO NA RAIS  WA ZAMANI  CHARLES TAYLOR Reviewed by safina radio on October 06, 2017 Rating: 5

No comments