RAIS WA TANZANIA JOHN MAGUFULI AMESEMA SERIKALI ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA WAWEKEZAJI .

TAREHE 31-10-2017

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amesema kuwa serikali itaendelea kushirikiana na wawekezaji mbalimbali wanaowekeza katika sekta ya viwanda ili kukuza uchumi wa nchi na kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

Mh Magufuli ametoa kauli hiyo leo wakati akizindua kiwanda cha kuzalisha bidhaa za Plastiki cha Vicktoria kilichopo eneo la Igogo wilayani Nyamagana Mkoani Mwanza,ambapo amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kukuza uchumi wake kupitia sekta ya viwanda hivyo itaendelea kushirikiana na wawekezaji hao ili azma hiyo iweze kufanikiwa.

Amesema kuwa kwa muda mrefu sekta ya viwanda hapa nchini imekuwa haifanyi vizuri kutokana na makosa aliyotendeka kipindi cha nyuma na kwa kutambua hilo serikali imeamua kurekebisha makosa hayo kwa kuanzisha viwanda vingi ambavyo vitasaidia kuwaajiri vijana wengi pamoja na kuchangia uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake waziri wa viwanda,biashara na uwekezaji Mh Charles Mwiijage amesema kuwa kiwanda hicho mbali na kusambaza bidhaa zake hapa nchini kinauza pia nje ya nchi na kusaidia taifa kupata fedha za kigeni na pia kimesaidia kuwaajiri wafanyakazi zaidi ya mia tano na kusaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.


Hata hivyo rais Magufuli yuko katika ziara ya siku mbili mkoani Mwanza,ambapo mbali na kuzindua kiwanda hicho cha plastiki amezindua pia kiwanda cha kutengenezea dawa za binadamu cha Prience Phamacetical Limited kilichopo wilayani Nyamagana mkoani humo.
RAIS WA TANZANIA JOHN MAGUFULI AMESEMA SERIKALI ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA WAWEKEZAJI . RAIS  WA  TANZANIA JOHN MAGUFULI  AMESEMA SERIKALI  ITAENDELEA KUSHIRIKIANA  NA WAWEKEZAJI . Reviewed by safina radio on October 31, 2017 Rating: 5

No comments