KIONGOZI WA KATALONIA AAPA KUTANGAZA UHURU WA JIMBO HILO

TAREHE 19-10-2017
CARLES PUIGDEMONT KUSHOTO NA WAZIRI MKUU WA UHISPANIA KULIA MARIANO RAJOY

Kiongozi wa Catalonia ameapa kwamba atatangaza uhuru, endapo serikali ya Uhispania italazimisha utawala wa moja kwa moja kutoka mjini Madrid.

Serikali kuu mjini Madrid imemtaka (Kales pugidemont) Carles Puigdemont kuachana na mipango ya kujitenga aliyoitangaza wiki iliyopita .
 Mzozo wa kisiasa umezidi kupamba moto tangu kufanyika kwa kura ya maoni ya tarehe 1 Oktoba, ambayo zaidi ya asilimia 90 ya Wakatalonia waliamua kuunda taifa lao, na ambayo Uhispania inasema haikuwa halali.

Hata hivyo hatua ya kuiondolea Catalonia mamlaka yake ya ndani iliyonayo inahitaji kura kwenye bunge la Uhispania, ambako chama cha Waziri Mkuu Mariano Rajoy kina wingi wa kutosha.
KIONGOZI WA KATALONIA AAPA KUTANGAZA UHURU WA JIMBO HILO KIONGOZI   WA   KATALONIA  AAPA  KUTANGAZA  UHURU  WA JIMBO HILO Reviewed by safina radio on October 19, 2017 Rating: 5

No comments