WAZIRI WA MAMBO YA NDANI MH. MWIGULU NCHEMBA AMEWASHUKURU WADAU WALIOJITOLEA KUJENGA NYUMBA ZA POLISI ZILIZOUNGUA MKOANI ARUSHA
TAREHE 17-10-2017
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mh Mwigulu Nchemba amewashukuru
wadau mbalimbali waliojitolea kujenga nyumba za askari polisi zilizoungua hivi
karibuni mkoani Arusha.
Akizungumza na wanahabari Mara baada ya kukagua
Ujenzi wa nyumba hizo mapema Leo Nchemba amesema kuwa wadau
waliojitolea katika Ujenzi huo wamefanya vyema ili kuharakisha
ukamilishaji wa nyumba hizo.
Amesema Rais wa nchi Mhe John Pombe Magufuli anatambua umuhimu
wa jeshi hilo ndio maana alitoa pesa ili kuhakikisha nyumba hizo zinajengwa
kwa haraka ambapo pia amemtaka mkuu wa Wilaya ya Arusha kumweleza mkuu wa
mkoa kuwa wanapaswa kupanga namna ya kukutana
ili kuangalia katika wizara ya mambo ya ndani jinsi ambavyo wanakwenda
kumalizia Ujenzi wa nyumba hizo.
Naye Kamanda wa polisi mkoani Arusha Charles Mkumbo amemshukuru
rais pamoja na wadau mbalimbali kwa namna walivyojitolea kuhakikisha askari
wanarudi kwenye makazi yao haraka iwezekanavyo kutokana na majengo hayo
kujengwa kwa haraka.
Hata hivyo kwa upande wa Mmoja wa wadau wanaojitolea katika
Ujenzi huo Hussain Gonga ambaye ni Mkurugenzi wa Tanzanite One amesema wameamua
kujitoa katika kusaidia Ujenzi huo kutokana nakutambua umuhimu wa jeshi
hilo ambapo amesema Usalama ndio kila kitu na wanaolinda Usalama ni askari
hivyo ni muhimu kukaa katika Mazingira bora.
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI MH. MWIGULU NCHEMBA AMEWASHUKURU WADAU WALIOJITOLEA KUJENGA NYUMBA ZA POLISI ZILIZOUNGUA MKOANI ARUSHA
Reviewed by safina radio
on
October 17, 2017
Rating:

No comments