Mlinda lango wa klabu ya West Brom Ben Foster aliumia kwenye goti akicheza na mwanawe kwenye bustani nyumbani kwao, meneja wa klabu hiyo Tony Pulis amesema.
Kipa huyo alikosa mechi ambayo West Brom walitoka sare ya 1-1 na Leicester siku ya Jumatatu.
Pulis alisema wana wasiwasi sana na kwamba wanasubiri uchunguzi zaidi kubaini ubaya wa jeraha hilo la goti.
Foster alikaa miezi 10 bila kucheza tangu Machi 2015 baada ya kuumia kano za goti.
FOSTER AUMIA AKICHEZA NA MWANAWE
Reviewed by safina radio
on
October 17, 2017
Rating: 5
No comments