RAIS WA TANZANIA MH.. JOHN MAGUFULI AWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU MAWAZIRI LEO

TAREHE 09-10-2017


Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli leo amewaapisha mawaziri na manaibu waziri baada ya kufanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri mwishoni mwa wiki.

Hafla ya kuwaapisha mawaziri hao imefanyika ikulu jijini Dar-es-salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo makamu wa rais Mh Samia Suluhu Hassan,waziri mkuu Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa,Spika wa Bunge Mh Job Ndugai,jaji mkuu wa Tanzania Mh Ibrahim Juma,makatibu wakuu,na viongozi wengine wa serikali na vyama vya siasa.

Akizungumza mara baada ya kuapishwa kwa mawaziri hao spika wa bunge Mh Job Ndugai amewapongeza wale wote walioteuliwa kushika nafasi hizo na kuwataka kwenda kufanya kazi kwa bidii kama walivyoaminiwa na Mh Rais, huku jaji mkuu Ibrahim Juma akiwataka mawaziri hao kufanya kazi 

kwa mujibu wa sheria ili pasije pakatokea mwingilano wa majukumu.
Naye Mh George Mkuchika ambaye ameapishwa kuwa waziri wa nchi ofisi ya rais utumishi na utawala bora amesema kuwa,katika majukumu yake atahakikisha watumishi wa umma wanafanya kazi kwa bidii na kuondoa urasimu katika maeneo ya kazi  kwa kuzingatia sheria na utawala bora.


Hata hivyo katika hafla hiyo jumla ya mawaziri walioapishwa ni 7 manaibu waziri 14 na katibu wa bunge mmoja ambaye ni Bw Steven Kigaigai.
RAIS WA TANZANIA MH.. JOHN MAGUFULI AWAAPISHA MAWAZIRI NA MANAIBU MAWAZIRI LEO RAIS  WA  TANZANIA  MH.. JOHN  MAGUFULI  AWAAPISHA MAWAZIRI  NA  MANAIBU  MAWAZIRI LEO Reviewed by safina radio on October 09, 2017 Rating: 5

No comments