VITUO VYA AFYA VIMEONYWA KUTOKUGHUSHI NYARAKA ZA MADAI
tarehe 06-10-2017
Vituo vya afya Mkoani Manyara
vimeonywa kutokughushi nyaraka za madai ya kupatiwa msaada kutoka mfuko wa bima
ya afya ulioboreshwa [ICHF] na badala yake vifuate sheria, kanuni na utaratibu
wa mfuko huo.
Wito huo umetolewa katika
mkutano mkuu wa wadau wa afya na Mkurugenzi wa mfuko wa bima ya
afya ulioboreshwa hapa nchini Bw. Hance Mwankenja,ambapo amesema kuwa mfuko huo
unahudumia Halmashauri saba za Mkoa wa Manyara
zenye jumla ya vituo 202 ambavyo ndani
yake kuna hospitali,zahanati na vituo vya afya.
Bw. Mwankenja amesema kuwa kumekuwa
na tabia ya vituo vinavyohudumiwa na mfuko huo kughushi nyaraka za madai kwa
lengo la kujipatia manufaa zaidi,hivyo amewaonya wamiliki wa vituo wenye tabia
kama hiyo kuacha mara moja la sivyo vituo hivyo vitafungiwa.
Aidha amesema kuwa kuna baadhi ya changamoto zinazowakabili
katika huduma wazozitoa ikiwemo
kutokuwepo kwa maabara katika vituo vingi vya serikali hali inayopelekea
wananchi kuhoji ukamilifu wa
matibabu huku changamoto
nyingine ikiwa ni vituo vingi
vinavyomilikiwa na serikali havina watumishi
na kama wapo wanakuwa
hawana sifa zinazohitajika
kukidhi mahitaji ya walengwa.
Hata hivyo ili kuhakikisha
mfuko huo unaendelea kuboresha huduma
zake umejipanga kusajili
maduka ya dawa vijijini ili kutatua
changamoto ya ukosefu wa dawa kwenye
vituo vya kutolea huduma ikiwa ni pamoja na kusajili maduka ya dawa
muhimu .
VITUO VYA AFYA VIMEONYWA KUTOKUGHUSHI NYARAKA ZA MADAI
Reviewed by safina radio
on
October 06, 2017
Rating:

No comments