RAIS WA BARAZA LA ULAYA DONALD TUSK AELEZEA MASHARTI YA UINGEREZA KUJITOA KATIKA UMOJA WA ULAYA
TAREHE 25-10-2017
Rais wa Baraza la Ulaya, Donald Tusk, ameyaelezea mazungumzo kuhusu
masharti ya Uingereza kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya, mchakato unaojulikana
kama Brexit, kuwa magumu na mtihani mkubwa kwa umoja huo.
Akizungumza leo wakati wa mjadala kwenye bunge la Umoja wa Ulaya,Tusk
amesema kwa mazungumzo ya Brexit, wamefanikiwa kujenga na kudumisha umoja
miongoni mwa nchi wanachama 27, lakini kilicho mbele yao bado ni kigumu na
mtihani mkubwa.
Pande zote hizo zimeshakutana mara
tano kukubaliana kuhusu masharti ya Uingereza kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya,
na mazungumzo mengine yamepangwa kufanyika katika kipindi cha miezi miwili
ijayo.
Wakati huo huo, Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Jean-Claude
Juncker, amesema umoja huo bado unafanya kazi ili kufikiwa makubaliano ''yenye
haki'' na Uingereza na kwamba kutofikiwa kwa makubaliano, sio dhana yao ya
kufanya kazi.
RAIS WA BARAZA LA ULAYA DONALD TUSK AELEZEA MASHARTI YA UINGEREZA KUJITOA KATIKA UMOJA WA ULAYA
Reviewed by safina radio
on
October 25, 2017
Rating:

No comments