ODINGA ATANGAZA KUJIONDOA KWENYE UCHAGUZI
TAREHE 11-10-2017
Marekebisho hayo yataruhusu mgombea anayesalia kuapishwa moja kwa moja.Mahakama ya juu nchini Kenya iliamuru uchaguzi mpya wa urais ufanywe baada ya kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa rais wa Agosti nane kwasababu ulikumbwa na dosari
Kinara
wa muungano wa upinzani nchini Kenya NASA Raila Odinga ametangaza kujiondoa
katika kinyanganyiro cha uchaguzi mpya wa urais uliopangwa kufanyika tarahe 26
mwezi huu, akihoji maafisa wa tume ya uchaguzi kwamba wameshindwa kufanya
mageuzi yanayohitajika.
Raila
amesema baada ya kutafakari msimamo wao kuhusiana na uchaguzi ujao, na kwa
kuzingatia maslahi ya Wakenya, kanda na ulimwengu kwa jumla wanaamini ni jambo
la busara kujiondoa kama mgombea urais katika uchaguzi huo.
Uamuzi
huo wa Raila unakuja wakati ambapo mswada uliowasilishwa bungeni na chama
tawala cha Jubilee kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta ukinuuia kuifanyia
marekebisho sheria ya uchaguzi ili kuepusha mzozo wa kisiasa iwapo kiongozi wa
muungano wa NASA Raila Odinga atajiondoa katika uchaguzi mpya wa urais katika
dakika ya mwisho.
Marekebisho hayo yataruhusu mgombea anayesalia kuapishwa moja kwa moja.Mahakama ya juu nchini Kenya iliamuru uchaguzi mpya wa urais ufanywe baada ya kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa rais wa Agosti nane kwasababu ulikumbwa na dosari
ODINGA ATANGAZA KUJIONDOA KWENYE UCHAGUZI
Reviewed by safina radio
on
October 11, 2017
Rating:

No comments