ZAIDI YA NYUMBA MIA MOJA ZAARIBIWA VIBAYA KUTOKANA NA MVUA MKOANI KATAVI

13-10-2017

Zaidi ya Kaya mia moja katika Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi hazina makazi baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali na kuezua paa na kubomoa  nyumba zao.

Mvua hizo zilizonyesha kwa muda wa siku mbili zimesababisha kujeruhiwa kwa wakazi watatu wa Manispaa hiyo.

Kata zilizoathirika na upepo huo ni Kazima,Kasese na Nsemulwa ambapo Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Katavi ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Meja Jenerali  Mstaafu Rafael Mhuga ametembelea maeneo hayo kwa lengo la kujionea uharibifu uliotoke.


Akiwa katika eneo hilo, Meja Jenerali Mstaafu Mhuga amebaini kuwapo kwa ujenzi usiozingatia maelekezo ya wataalamu wa Mipango Miji na hivyo kuwa chanzo cha kuharibika kwa nyumba hizo .
ZAIDI YA NYUMBA MIA MOJA ZAARIBIWA VIBAYA KUTOKANA NA MVUA MKOANI KATAVI ZAIDI  YA NYUMBA MIA MOJA  ZAARIBIWA VIBAYA  KUTOKANA  NA MVUA  MKOANI KATAVI Reviewed by safina radio on October 13, 2017 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.