ODINGA AITISHA MAANDAMANO KUSHINIKIZA MAGEUZI KATIKA TUME YA UCHAGUZI IEBC

TAREHE 29-09-2017
KIONGOZI  WA UPINZANI NCHINI KENYA RAILA ODINGA
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga, ametangaza jana kuwa ataitisha maandamano kushinikiza mageuzi ndani ya tume ya uchaguzi na kukizuwia chama tawala kuondoa kinga dhidi ya udanganyifu kuelekea uchaguzi mpya wa rais.

 Odinga ameitisha maandamano ya nchi nzima wiki ijayo, baada ya mazungumzo kuvunjika jana kati ya tume ya uchauguzi, chama tawala cha Jubilee, na wawakilishi wake, juu ya namna ya kufanya uchaguzi mpya wa rais.

Tume ya uchaguzi IEBC ilitangaza tarehe 26 Oktoba kuwa siku ya uchaguzi mpya, baada ya mahakama ya juu kabisa nchini humo kubatilisha ushindi wa rais Uhuru Kenyatta kutokana na kukosekana kwa uhakiki wa matokeo.


 Odinga anasema wadukuzi waliingilia mitambo ya kurusha matokeo ya tume ya uchaguzi na kubadilisha matokeo.
ODINGA AITISHA MAANDAMANO KUSHINIKIZA MAGEUZI KATIKA TUME YA UCHAGUZI IEBC ODINGA  AITISHA  MAANDAMANO   KUSHINIKIZA  MAGEUZI   KATIKA  TUME  YA UCHAGUZI IEBC Reviewed by safina radio on September 29, 2017 Rating: 5

No comments