BUNGE LA TUNISIA LAPITISHA SHERIA TATA ILI KUTOA MSAMAHA KWA WATU WANAOHUSISHWA NA MAKOSA YA RUSHWA
![]() |
WABUNGE WA TUNISIA WAKIWA KWENYE KIKAO |
Bunge la Tunisia limepitisha sheria tata inayolenga kutoa msamaha kwa maelfu ya watu nchini humo wanaohusishwa na rushwa, chini ya utawala wa kidikteta kabla ya vuguvugu la mapinduzi ya umma.
Baadhi ya
watu waliandamana nje ya bunge hilo kupinga hatua hiyo wakisema wanahofia
kuirudisha Tunisia katika enzi za kabla ya vuguvugu la mabadiliko.
Baada ya
mjadala wa hasira na kutoka nje kwa wabunge wa upinzani, sheria hiyo
ilipitishwa kwa kura 117 zilizounga mkono huku kura tisa zikipinga.
Rais wa nchi
hiyo mwenye umri wa miaka 90 anasema sheria hiyo ya maridhiano ya kiuchumi
itaboresha mazingra ya uwekezaji na kuiwezesha nchi hiyo kupiga hatua.
Msamaha kamili
chini ya sheria hiyo utawahusu wale waliotekeleza amri kutoka kwa viongozi
mafisadi lakini ambao hawakunufaika binafsi kutokana na hatua hizo walizochukua
huku wale waliojipatia fedha kwa njia ya rushwa watalazimika kurejesha fedha
hizo pamoja na faini ili kuepukana na kushitakiwa.
BUNGE LA TUNISIA LAPITISHA SHERIA TATA ILI KUTOA MSAMAHA KWA WATU WANAOHUSISHWA NA MAKOSA YA RUSHWA
Reviewed by safina radio
on
September 14, 2017
Rating:

No comments