HALMASHAURI YA WILAYA YA HANANG MKOANI MANYARA IMEFANIKIWA KUTATUA MGOGORO KATI YAKE NA WIZARA YA NISHATI MADINI .
TAREHE 19-09-2017
![]() |
KAMISHINA MSAIDIZI WIZARA YA NISHATI NA MDINI KANDA YA KASKAZINI BW. ADAM JUMA |
Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’ iliyopo mkoani Manyara
imefanikiwa kutatua mgogoro uliokuwa ukiendelea kati yao na wizara ya
nishati na madini kanda ya kasikazini uliokuwa ukihusiana na utozwaji wa
ushuru katika mgodi wa chumvi uliopo katika kata ya Gendabi
wilayani humo.
Akizungumza katika mkutano na wakazi wa vijiji vya Gendabi,Sebasi,Hargushay
na Sarjanda vyote vikiwa vinaunda kata ya Gendabi Kamishina msaidizi
wa wizara ya nishati na madini kanda ya kasikazini Bw.Adam Juma
alieleza kuwa mgogoro huo ulitokana na fedha zilizokuwa zikitolewa
na serikali kwa ajili ya kusaidia vikundi vidogo vidogo vya uchimbaji wa
madini kwa ajili ya kuwakwamua na kuwapa ari ya kufanya
kazi.
Amesema kuwa jumla ya vikundi 59 vilivyosajiliwa
hapa nchini vimenufaika na fedha hizo za serikali huku mkoa Wa manyara
ukijwa kuwa na vikundi 6 ambapo kukindi kimojawapo ni cha uchimbaji
wa chumvi katika mgondi wa chumvi wa Hargushay kinachofahamika kwa majina
ya Hasami kinachochimba chumvi katika mgondi huo pamoja na kuuza.
Naye mkuu wa wilaya ya Hanang’ Sarah Msafiri amesema
chumvi inayozalishwa katika mgondi huo imekuwa ikisafirishwa kwenda
nchi za Rwanda,Burundi,Kenya na Malawi kwa ajili ya matumizi
mabalimbali lakini mafanikio ni kidogo ikilinganishwa na uchimbaji
unaofanywa katika mgondi huo na hiyo ni kutokana na kukosa usimamizi wa kukusanya
mapato katika njia zilizosahihi.
HALMASHAURI YA WILAYA YA HANANG MKOANI MANYARA IMEFANIKIWA KUTATUA MGOGORO KATI YAKE NA WIZARA YA NISHATI MADINI .
Reviewed by safina radio
on
September 19, 2017
Rating:

No comments