Taarifa ya habari 13 sept 2017 saa 7:00 mchana
DODOMA.
Waziri wa
afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Ummy Mwalimu amesema kuwa
serikali imeongeza vituo 150 kwa ajili ya kutoa huduma za uzazi wa dharura ili
kuokoa vifo vitokanavyo na uzazi pingamizi.
Mh Mwalimu
ameyasema hayo katika kikao cha wabunge wa klabu ya uzazi salama,ambapo amesema
kuwa katika kufanikisha suala hilo serikali imeandaa fedha kwa ajili ya kujenga
vituo vitano vya kuhifadhia damu salama kwa ajili ya upasuaji wa wanawake
wanapojifungua.
Amesema kuwa
serikali pia imeongeza bajeti ya uzazi salama kutoka bilioni 16 hadi bilioni
32,ambapo kwa sasa ni vituo vya afya vya serikali mia moja ishirini tu
vinavyotoa huduma ya uzazi wa dharura hivyo serikali ameamua kuongeza vituo
vingine mia moja hamsini ili vifikie mia mbili tisini kati ya mia tano hamsini
na sita vinavyotakiwa.
Hata hivyo
takwimu zinaonyesha kuwa,katika kila wanawake laki moja hapa nchini wanawake
mia tano hamsini na sita wanaojifungua hupoteza maisha kila mwaka kutokana na
uzazi.
.........................................................................................................................
ARUSHA.
Mkuu wa mkoa
wa Arusha Bw Mrisho Gambo amemwagiza mkurugenzi wa halamashauri ya Arusha na
katibu tawala wake kutafuta ufumbuzi wa tatizo la wananchi kutozwa fedha kwa
ajili ya kupimiwa ardhi ili waweze kupewa hati za kimila.
![]() |
Mkuu wa mkoa wa Arusha Bw Mrisho Gambo |
Bw Gambo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi wa kitongoji Ingorora na pasiliani kata ya Kisongo katika halmashauri ya Arusha akiwa katika ziara ya siku tano yenye lengo la kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi,ambapo amesema kuwa ni lazima majibu sahihi yatolewe ili kuweza kufahamu undani wa suala hilo.
Amesema kuwa
haiwezekani jambo lifanywe na serikali wananchi wachangishwe fedha na jambo
hilo lisieleweke hivyo mkurugenzi pamoja na katibu wanatakiwa kufuatilia tatizo
hilo na kisha kuwasilisha majibu yake kwake kwa njia ya maandishi na ameahidi
kurudi tena katika kata hiyo kufuatilia majibu ya maagizo aliyoyatoa.
Hata hivyo
mkuu wa mkoa wa Arusha yupo katika ziara ya siku tano katika halmashauri ya
Arusha ikiwa ni utaratibu wake aliojiwekea ya kutembelea wilaya na halmashauri
zote za mkoa wa Arusha lengo likiwa ni kusikiliza na kutatua kero mbalimbali
zinazowakabili wananchi.
..........................................................................................................................
DODOMA.
Naibu waziri
wa fedha na mipango Dr Ashantu Kijaji amesema kuwa lengo la serikali kuamua
kukusanya kodi za majengo katika halmashauri na majiji hapa nchini ni ili
kuongeza mapato mengi zaidi yatakayosaidia kuwaletea wananchi wa hali ya chini
maendeleo.
![]() |
DR Ashantu Kijaji. |
Dr Kijaji ameyaseama hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalumu Mh Cecilia Pareso aliyetaka kujua serikali kuu imefanikiwa kukusanya kiasi gani cha fedha kuanzia ilipoanza kukusanya kodi za majengo katika halmashauri na majiji hapa nchini.
Amesema kuwa
ili kuondoa kero mbalimbali zinazowakabili wananchi ni lazima serikali ipate
mapato ya kutosha,ambapo katika mwaka wa fedha wa 2015/16 na 2016/17 mamlaka ya
mapato Tanzania imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 34 katika
halmashauri,manspaa na majiji 30 hapa nchini tofauti na hapa awali ambapo
ukusanyaji ulikuwa ni shilingi bilioni 28 pekee.
Ameongeza
kuwa,fdha zinazopatikana katika makusanyo hayo zinapelekwa katika halmashauri
ili ziweze kutatua kero za wananchi kama ilivyo azma ya serikali ya awamu ya
tano kuwahudumia wananchi wa hali ya chini ili waweze kuondokana na umaskini na
kufikikia uchumi wa kati ifikapo mwaka wa 2025.
Hata hivyo
bunge la kumi na moja mkutano wa nane unaendelea mjini Dodoma,ambapo pamoja na
mambo mengine wabunge watajadili na kupitisha miswada mitatu ya sheria na bunge
hilo litahitimishwa Septemba 15 mwaka huu.
.............................................................................................................
KIMATAIFA .
NAIROBI.
Polisi nchini Kenya wamewakamata watu wanne wanaoaminika kuwa raia wa Burundi ambao walikuwa wakielekea Somalia kujiunga na kundi la al-Shabab.
![]() |
polisi nchini Kenya wakamata raia wa burundi |
Msemaji wa poli nchini Kenya George Kinoti amesema kuwa maafisa wa ujasusi walikuwa wakiwafuata washukiwa hao baada ya kupata habari kuhusu mipango yao.
Ameongeza kwamba washukiwa wanne walikamatwa katika kizuizi cha polisi mjini Isiolo takriban kilomita mia tatu hamsini kaskazini mwa mji mkuu wa Nairobi wakielekea katika mji wa mpakani wa Mandera.
Maafisa wa polisi pia wanasema wanne hao waliingia nchini Kenya kama watalii kupitia visa huru ya ushirikiano kati ya Burundi na Kenya.
Maafisa katika Ubalozi wa Burundi mjini Nairoibi wanasema kuwa watatoa taarifa kamili kuhusu kukamatwa huko baada ya kushauriana na mamlaka ya Kenya.
...................................................................................................................................................................
PYONGYANG.
Korea Kaskazini imeapa leo kuuharakisha mpango wake wa
silaha za nyuklia kama hatua ya kujibu vikwazo ilivyowekewa na baraza la
usalama la Umoja wa Mataifa baada ya jaribio lake la sita na kubwa kabisa la
silaha za nyuklia.
Wizara ya mambo ya nchi za kigeni ya Korea Kaskazini
imesema katika taarifa kwamba taifa hilo litaongeza maradufu juhudi za
kujiimarisha ili kuulinda uhuru na haki yake.
Vikwazo vipya vilivyoandaliwa na Marekani vilipitishwa
siku ya Jumatatu na vinajumuisha marufuku ya kuuza nguo katika nchi za nje na
kudhibiti usafirishaji wa bidhaa za mafuta kuuadhibu utawala wa Pyongyang kwa
jaribio hilo.
Rais wa Marekani Donald Trump amesema hatua kali zaidi
zinahitajika kuchukuliwa dhidi ya Korea Kaskazini baada ya vikwazo vipya vya
Umoja wa Mataifa.
.........................................................................................................................
CARACAS.
Rais wa
Venezuela Nicolas Maduro amesema yuko tayari kukutana na upinzani kwa
mazungumzo yanayosimamiwa na Jamhuri ya Dominican na waziri mkuu wa zamani wa
Uhispania Jose Luis Rodriguez Zapatero.
Waziri wa
mashauri ya kigeni wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesema serikali ya Venezuela
itafanya awamu ya kwanza ya mazungumzo
katika Jamhuri ya Dominican leo.
Akizungumza
baada ya kukutana na waziri wa mambo ya nchi za nje wa Venezuela Jorge Arreaza
mjini Paris, Le Drian amesema mazungumzo hayo yanasimamiwa na rais Danilo Medina
wa Jamhuri ya Dominican na waziri mkuu wa zamani wa Uhispania Jose Luis
Rodriguez Zapatero.
Le Drian ameonya Venezuela huenda ikawekewa
vikwazo na Umoja wa Ulaya iwapo haitashiriki mazungumzo hayo,ambapo pua Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema anayaunga mkono kikamilifu
mazungumzo hayo.
Endelea kufuatilia ukurasa wetu kwa habari mbalimbali saa saba na saa mbili usiku. mshirikishe na mwenzako
Taarifa ya habari 13 sept 2017 saa 7:00 mchana
Reviewed by safina radio
on
September 13, 2017
Rating:

No comments