MKANDARASI ANAYEJENGA DARAJA LA MLALAKUWA JIJINI DAR ES SALAAM AAGIZWA KUKAMILISHA MRADI HUO

TAREHE 26-09-2017

WAZIRI WA UJENZI,MIUNDOMBINU NA MAWASILIANO MH. MAKAME  MBARAWA  MNYAA

Waziri wa ujenzi,miundombinu na mawasiliano Mh Makame Mbarawa Mnyaa amemwagiza mkandarasi anayejenga daraja la Mlalakuwa jijini Dar-es-salaam kukamilisha mradi huo ifikapo mwezi Desemba mwaka huu.

Mh Mbarawa ametoa maagizo hayo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo,ambapo amesema kuwa mradi huo ni sehemu ya upanuzi wa barabara ya Mwai Kibaki Old Bagamoyo yenye urefu wa kilomita 5.3 na umekamilika kwa asilimia 42 hadi sasa.

Kwa upade wake mhandisi wa miradi ofisi ya meneja mkoa wa Dar-es-salaam Bw Julias Ngusa amemwakikishia waziri Mbarawa kuwa mradi huo utakamilika katika kipindi kilichopangwa licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa katika ujenzi huo.


Hata hivyo daraja hilo lilianzwa kujengwa tarehe 25 Octoba mwaka wa 2016 na mpaka sasa umekamilika kwa asilimia 42 katika kipindi cha miezi 10.
MKANDARASI ANAYEJENGA DARAJA LA MLALAKUWA JIJINI DAR ES SALAAM AAGIZWA KUKAMILISHA MRADI HUO MKANDARASI   ANAYEJENGA  DARAJA   LA  MLALAKUWA   JIJINI  DAR ES SALAAM  AAGIZWA  KUKAMILISHA    MRADI   HUO Reviewed by safina radio on September 26, 2017 Rating: 5

No comments