RAIS MPYA WA ANGOLA KUAPISHWA LEO

TAREHE 26-09-2017

RAIS MPYA WA ANGOLA JOAO LOURENCO

Rais mpya wa Angola anatarajiwa kuapishwa leo Jumanne hii ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika mabadiliko katika uongozi wa taifa hilo katika kipindi cha miongo karibu minne.


João Lourenço, aliyekuwa waziri wa ulinzi anachukuwa nafasi ya Jose Eduardo Dos Santos rais anayeondoka ambaye aliamua kuachia madaraka baada ya kuongoza nchini hiyo miaka 38.

Mwandishi mmoja wa habari nchini humo amesema kuwa watu wa Angola wanaunga mkono mabadiliko lakini huenda kusishuhudiwe  mabadiliko makubwa kwa sababu Bw Lourenço amekuwa mwandani wa karibu wa chama tawala, ( Popular Liberation Movement of Angola MPLA) kwa miongo kadhaa.

Dos Santos atasalia kuwa kiongozi wa chama hicho ambaye ana haki ya kumteua mkuu wa majeshi na polisi.

Chama cha MPLA kimeongoza Angola tangu ilipojinyakulia uhuru wake kutoka kwa Mreno mwaka 1975
RAIS MPYA WA ANGOLA KUAPISHWA LEO RAIS   MPYA  WA   ANGOLA   KUAPISHWA   LEO Reviewed by safina radio on September 26, 2017 Rating: 5

No comments