MKUU WA MKOA WA KAGERA MEJA MSTAAFU SALIM KIJUU AMETOA MUDA WA WIKI MOJA KWA HALMASHAURI ZOTE ZA MKOA HUO KUNYUNYIZIA DAWA ZA VIWATILIFU VYA MALARIA.
TAREHE 18-09-2017
![]() |
MKUU WA MKOA WA KAGERA MEJA MSTAAFU SALIM KIJUU |
Mkuu wa mkoa
wa Kagera Meja mstaafu Salim Kijuu ametoa muda wa wiki moja kwa halmashauri
zote za mkoa huo kuhakikisha kuwa zinanyunyizia dawa za viwatilifu vya malaria
zilizotolewa na serikali tangu mwezi Juni mwaka huu katika nyumba za wananchi
wa wilaya hizo.
Brigedia
Kijuu ametoa maagizo hayo katika kikao cha wadau kilicholenga kupanga mikakati
ya kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa malaria mkoani humo,ambapo maambukizi
yamepanda kwa asilimia 35 katika kipindi cha miaka mitano iliyopita mkoani humo.
Amesema kuwa
hategemei kuona dawa zilizotolewa na serikali kwa ajili ya kuulia mbu
zinahifadhiwa katika magala kwa kuwa maeneo yanayotakiwa kunyunyiziwa dawa hizo
yapo mengi ikiwemo madimbwi kwani lengo la serikali kutoa madawa hayo ni kuua
mbu wanaowasumbua wananchi na kusababisha vifo hapa nchini.
Kwa upande
wake mratibu wa ugonjwa wa malaria mkoa wa Kagera Dr Julian Mgengi amesema kuwa
licha ya juhudi mbalimbali kufanyika ikiwemo ugawaji wa vyandarua na unyunyiziaji
wa dawa ya mkoko majumbani bado elimu inatakiwa kuendelea kutolewa ili wananchi
wafahamu madhara zaidi yatokanayo na ugonjwa wa malaria.
Hata hivyo
wilaya zitakazonufaika na zoezi hilo ni pamoja na Ngara,Misenyi na Bukoba
vijijini ambazo kitakwimu inaonesha kuwa maambukizi ya malaria yamepungua
kutokana na unyunyiziaji wa dawa uliofanyika mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka
huu.
MKUU WA MKOA WA KAGERA MEJA MSTAAFU SALIM KIJUU AMETOA MUDA WA WIKI MOJA KWA HALMASHAURI ZOTE ZA MKOA HUO KUNYUNYIZIA DAWA ZA VIWATILIFU VYA MALARIA.
Reviewed by safina radio
on
September 18, 2017
Rating:

No comments