MATOKEO LIGI YA MABINGWA ULAYA
TAREHE 27-09-2017
![]() |
HARRY KANE |
Harry Kane amekuwa
mchezaji wa saba wa Kiingereza kufunga hat-trick kwenye michuano ya Ligi ya
Mabingwa katika mechi ya Jumanne waliyocheza dhidi ya APOEL Nicosia.
Mshambuliaji huyo wa
Tottenham Hotspur aliifungia timu yake magoli katika ushindi huo wa Cyprus,
akiweka kimiani kwa kila mguu na moja la kichwa.
Kane, 24, sasa
amefikia mafanikio ya Waingereza wenzake Andrew Cole, Michael Owen, Wayne
Rooney, Alan Shearer, Danny Welbeck na Mike Newell.
Kwingineko Monaco wameangukia pua
mikononi mwa Porto kwa kichapo cha 3-0 katika mechi ya Jumanne usiku Ligi ya
Mabingwa Ulaya kwenye uwanja wa Stade Louis II.
Wenyeji hao walikuwa wa kwanza kuanza
kuleta balaa langoni mwa Porto Radamel Falcao akijaribu kufunga ikiwa ni dakika
ya nne tangu mchezo uanze.
Porto walipata goli lao la kwanza dakika
ya 31 Vincent Aboubakar alipopiga shuti
kali lililomshinda Diego Benaglio ambaye aliokoa michomo mingi.
Goli la pili kwa wageni hao lilipatikana
dakika ya 69 pale Moussa Marega alipompa pasi nzuri Aboubakar ambaye
aliunganisha moja kwa moja hadi wavuni Porto wakiandika bao la pili.
Kikosi cha Sergio Conceicao
kiliongeza goli la tatu dakika moja kabla ya mechi kumalizika Marega
alipomchongea pasi matata Miguel Layun aliyetokea benchi na kumaliza mchezo kwa
ushindi wa mabao matatu.
Majogoo wa jiji Liverpool wameendelea
kusubirishwa kupata ushindi wa kwanza Ligi ya Mabingwa msimu huu baada ya
kushikiliwa kwa sare ya 1-1 dhidi ya Spartak Moscow.
Walikuwa wenyeji walioanza kupata goli
la kuongoza kupitia mpira wa adhabu uliopigwa na Fernando, lakini pia Liverpool
nao walishindwa kumiliki mpira vizuri na kutengeneza nafasi.
Philippe Coutinho aliisawazishia
Liverpool, lakini hawakuweza kuongeza goli la pili na wakapoteza pointi mbili
tena kwenye kundi E baada ya kushikiliwa kwa sare na Sevilla mechi iliyopita.
Mechi nyingine Gareth Bale alifungua
ukurasa wa mabao akiifungia Real Madrid katika uwanja wa Signal Iduna Park
kabla ya Ronaldo kufunga mara mbili.
Nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo
amewajibu vidomo-domo huku akiwashangaza kwa kiwango safi.Mabao mawili ya Ronaldo
yaliisaidia Madrid kushinda 3-1 dhidi ya Borussia Dortmund kwenye Ligi ya
Mabingwa Ulaya Jumanne.
Nyota huyo hajarudi vizuri kwenye mechi
za Ligi, kwani hajafanikiwa kufunga kwenye mechi mbili za La Liga tangu amalize
adhabu yake.
MATOKEO LIGI YA MABINGWA ULAYA
Reviewed by safina radio
on
September 27, 2017
Rating:

No comments