WAZIRI MKUU WA UHISPANIA MARIANO RAJOY ANATARAJIA KWENDA KATIKA JIMBO LINALOTAKA KUJITENGA LA CATALONIA



TAREHE 15 -09-2017

WAZIRI MKUU WA UHISPANIA MARIANO RAJOY

Waziri Mkuu wa Uhispania, Mariano Rajoy leo anatarajiwa kwenda katika jimbo linalotaka kujitenga la Catalonia, kutokana na hatua mpya ya viongozi wa kundi linalotaka kujitenga kuanzisha kampeni yao kuhusu kura ya maoni ya uhuru.

Jana jioni, Rais wa Catalonia Carles Puigdemont akiwa mbele ya viongozi wengine wa kundi linalotaka kujitenga, pamoja na umati wa wafuasi 8,000 waliokusanyika Tarragona, alitangaza kuanza rasmi kwa kampeni hiyo ya kura ya maoni ambayo imepigwa marufuku na serikali ya Uhispania.

 Rajoy anatarajiwa kukutana na wanachama wa chama chake cha kihafidhina cha Popular mjini Barcelona na hatarajiwi kuhutubia umati wowote wa watu.


 Hata hivyo zaidi ya asilimia 70 wamesema wanataka kufanyika kwa kura hiyo ya maoni. Meya wa Barcelona, Ada Colau amesema kura hiyo itaruhusiwa kufanyika bila kujali uamuzi wa serikali kuu mjini Madrid.
WAZIRI MKUU WA UHISPANIA MARIANO RAJOY ANATARAJIA KWENDA KATIKA JIMBO LINALOTAKA KUJITENGA LA CATALONIA WAZIRI  MKUU  WA  UHISPANIA  MARIANO  RAJOY  ANATARAJIA  KWENDA  KATIKA  JIMBO  LINALOTAKA  KUJITENGA  LA  CATALONIA Reviewed by safina radio on September 15, 2017 Rating: 5

No comments